![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/14/Gabon_-_Estuaire.svg/langsw-640px-Gabon_-_Estuaire.svg.png&w=640&q=50)
Mkoa wa Estuaire
From Wikipedia, the free encyclopedia
Estuaire ni moja kati ya mikoa tisa ya nchini Gabon. Mkoa umechukua eneo la kilomita za mraba zipatazo 20,740. Mji mkuu wa mkoa huu ni Libreville, ambayo pia ndiyo mji mkuu wa nchi. Mkoa umepewa hili kwa ajili ya Mlango wa Mto wa Gabon, ambao ndiyo moyo wa mkoa huu.
![Estuaire Province](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/14/Gabon_-_Estuaire.svg/640px-Gabon_-_Estuaire.svg.png)
![]() | Makala hii, au sehemu za makala hii, inahitaji vyanzo au marejeo yoyote. Tafadhali saidia kuboresha makala hii kwa kuweka vyanzo vya kuaminika. Habari zisizowekewa vyanzo zinaweza kuwekewa alama na kuondolewa. (Desemba 2008) |
Ukingo wa magharibi mwa Estuaire ni pwani ya Ghuba ya Guinea. Kwa upande wa kaskazini, Estuaire imepakana na Jamhuri ya Guinea ya Ikweta: Mkoa wa Litoral kwa upande wa kaskazini-magharibi, na Mkoa wa Centro Sur kwa upande wa kaskazini-mashariki. Kwa nyumbani, mkoa umepakana na mikoa ifuatayo:
- Woleu-Ntem - mashariki
- Moyen-Ogooué - kusini
- Ogooué-Maritime - kusini-magharibi