Ghuba ya Guinea

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ghuba ya Guinea

Ghuba ya Guinea ni kidaka kikubwa cha bahari ya Atlantiki kwenye pwani ya magharibi mwa Afrika.

Ramani ya Ghuba ya Guinea.

Eneo lake linahesabiwa kuanza nchini Liberia kwenye rasi ya Palmas na kwisha kwenye rasi Lopez nchini Gabon.

Jina la "Guinea" limetokana na jina la kale la sehemu kubwa ya upande wa kusini wa Afrika ya Magharibi kati ya jangwa la Sahara na Atlantiki likimaanisha "nchi ya watu weusi" kwa lugha ya Kiberber.

Kati ya mito mikubwa inayoishia kwenye ghuba hiyo ni Niger, Volta na Kongo.

Mwambao wa ghuba una vidaka viwili vidogo ambavyo ni hori ya Benin na hori ya Biafra (Nigeria imebadilisha jina hili kuwa hori ya Bonny baada ya vita vya Biafra).

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.