Mbwigu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mbwigu ni ndege wakubwa kiasi wa familia Laniidae. Wanatokea Afrika, Asia na Ulaya kwa muhimu, spishi mbili tu huzaa huko Amerika ya Kaskazini. Ndege hawa ni mweusi na mweupe kwa kawaida, mara nyingi wana rangi ya kijivu, kahawa na nyekundu pia. Wana domo nene lenye ncha kwa kulabu na spishi nyingi zina mkia mrefu. Hula wadudu na vertebrata wadogo (mijusi, panya, ndege n.k.) na huwa na tabia ya kuwafumia mwiba. Mwiba unafaa kama akiba na ili kushikilia windo wakati mbwigu akichana vipande. Hulijenga tago lao kwa vijiti na nyasi mtini au kichakani. Jike huyataga mayai 3-9.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Mbwigu | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mbwigu barabara | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Funga