Kunguru
Ndege wa familia Corvidae / From Wikipedia, the free encyclopedia
Kunguru ni ndege wakubwa kiasi wa familia Corvidae. Spishi nyingine huitwa vinubi. Wanatokea mabara yote isipokuwa Antakitiki. Spishi nyingi ni nyeusi au nyeusi pamoja na rangi ya nyeupe, kijivu au kahawa; nyingine zina rangi mbalimbali kama buluu, pinki n.k. Hula nusra kila kitu: wanyama na ndege wadogo, wadudu, mizoga, matunda, nafaka n.k. Hulijenga tago lao kwa vijiti juu ya mti au jabali. Spishi nyingine huyajenga matago kwa makundi. Jike huyataga mayai 3-10.
Kunguru | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kunguru Shingo-kahawia | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||