Maulid
From Wikipedia, the free encyclopedia
Maulid (pia: maulidi, kwa kirefu: Maulid an-Nabii) ni sikukuu ya dini ya Uislamu ya kuadhimisha kuzaliwa kwake Mtume Muhammad takriban mwaka 570 BK.
Neno lenyewe ni la asili ya Kiarabu kutokana na مولد النبي , maulid an-nabi, au ميلاد النبي , milaad an-nabi). Sikukuu inafuata kalenda ya Kiislamu. Waislamu wa dhehebu la Sunni husheherekea tarehe 12 Rabi'-ul-Awwal kwa mujibu ya kalenda ya Kiislamu ya Alhijria na Waislamu wa dhehebu la Shia husheherekea tarehe 17 Rabi'-ul-Awwal.
Wataalamu wa historia wengine wanasema ya kwamba sherehe ya Maulid imeanzishwa mnamo karne ya 12 BK. Kuna Waislamu kadhaa wanaokataa sherehe hiyo kwa sababu hakuna sunna wala hadith ya Muhammad mwenyewe kuhusu kusheherekea maulid yake. Lakini kwa ujumla ni sikukuu inayopendwa sana na Waislamu wengi duniani. Misri maulid ni kati ya sikukuu za Kiislamu zinazokumbukwa sana na Waislamu. Katika Afrika ya Mashariki sherehe ya maulid huko Lamu imejulikana hasa ikivuta wageni kutoka pande zote za Afrika ya Mashariki hadi Uarabuni.
Kati ya desturi ni mikutano, kusikia mashairi juu ya maisha ya mtume a mengine.