Lanthanidi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lanthanidi au lanthanoidi (Kiingereza: lanthanides au lanthanoids) ni kundi la elementi za kimetali zenye namba atomia kutoka 57 hadi 71, ambazo tabia zake zinafanana. Elementi hizo huhesabiwa kati ya madini adimu kama vile monaziti. Kundi hilo huanza na lanthani na kuishia kwa luteti. [1] [2]
Namba atomia | Elementi ya kikemia | Alama | Picha |
---|---|---|---|
57 | Lanthani | La | |
58 | Ceri | Ce | |
59 | Praseodimi | Pr | |
60 | Neodimi | Nd | |
61 | Promethi | Pm | ā |
62 | Samari | Sm | |
63 | Europi | Eu | |
64 | Gadolini | M-ngu | |
65 | Terbi | Tb | |
66 | Disprosi | Dy | |
67 | Holmi | Ho | |
68 | Erbi | Er | |
69 | Thuli | Tm | |
70 | Ytebi | Yb | |
71 | Luteti | Lu |
Lanthanidi ni metali zinazofanana katika tabia nyingi. Nyingi hubadilika polepole kuwa hidroksidi zake wakati zimewekwa ndani ya maji, sawa na metali alikali.
Hewani huunda kwa kawaida ganda jembamba la oksidi wakati sawa na metali nyingi. Lanthanidi, pamoja na skandi na ytri, huhesabiwa kati ya elementi za ardhi adimu. Lanthanidi zote ni metali nyeupe na laini zinazobadilisha rangi ya nje haraka zikiathiriana na hewa. Ugumu wake huongezeka sambamba na namba atomia.
Lanthanidi hazipatikani wala hazichimbwi kwa viwango vikubwa.