Lanthani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lanthani ni elementi ya kikemia yenye alama ya La. Namba atomia ni 57. Ni sehemu ya kundi la elementi za Lanthanidi ikihesabiwa kati ya ardhi adimu. Rangi yake ni kidhahabu - nyeupe, lakini hewani inapata haraka ganda la oksidi lenye rangi ya kijivu. Ni laini na inaweza kukatwa kwa kisu.
Ukweli wa haraka Lanthani (Lanthanum) ...
Lanthani (Lanthanum) | |
---|---|
Jina la Elementi | Lanthani (Lanthanum) |
Alama | La |
Namba atomia | 57 |
Uzani atomia | 138.905 |
Valensi | 2, 8, 18, 18, 9, 2 |
Densiti | 6.126 g/cm3 |
Ugumu (Mohs) | 2.5 |
Kiwango cha kuyeyuka | 1193 K (920 °C) |
Kiwango cha kuchemka | 3737 K (3464 °C) |
Asilimia za ganda la dunia | 17 ppm |
Hali maada | mango |
Funga
Jina linatokana na Kigiriki λανθάνειν lanthanein (kuficha) kwa sababu wanakemia walioitambua katika karne ya 19 waliona ugumu kuitenganisha na madini mengine.
Kuna matumizi ya lanthani katika teknolojia mbalimbali:
- "jiwe la kiberiti" huwa na asilimia 25-45 za lanthani
- wakala nakisishi (kiungo cha kuondosha oksijeni) katika uzalishaji wa aloi za metali
- inaungwa katika chuma ili kuongeza ufulikivu uzi
- oksidi ya lanthani huungwa katika kioo cha lenzi za kamera
- lanthani hutumiwa katika beteri za magari ya umeme aina ya NiMH; [1]