Kaizari Valerian
From Wikipedia, the free encyclopedia
Publius Licinius Valerianus (takriban 193/200 – 260/264) alikuwa Kaizari wa Dola la Roma kuanzia tarehe 22 Oktoba 253 hadi 260 alipotekwa na mfalme Shapur I wa Uajemi. Jambo hilo jipya lilitikisa dola lote.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/dc/Aureus_Valerian-RIC_0034-transparent.png/320px-Aureus_Valerian-RIC_0034-transparent.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a2/HumiliationValerianusHolbein.jpg/640px-HumiliationValerianusHolbein.jpg)
Wakati alipoandaa vita yake dhidi ya Uajemi aliamuru sadaka kwa miungu ya Roma zitolewe pia na Wakristo. Aliposikia kwamba walikataa aliagiza kuua maaskofu; Wakristo wengine waliokuwa na cheo walipoteza cheo na mali na kuuzwa kama watumwa wakikataa sadaka hiyo[1]. Alitawala pamoja na mwana wake, Kaizari Galienus. Baada ya kifo cha baba yake, Galienus alisimamisha dhuluma dhidi ya Wakristo. Alimfuata Aemilianus.