From Wikipedia, the free encyclopedia
Kihispania (español; Kiingereza: Spanish) ni lugha ya kimataifa ambayo ni lugha ya kwanza kwa watu milioni 493; kwa jumla pamoja na wasemaji wa Kihispania kama lugha ya pili kuna milioni 568 duniani wanaosema vizuri Kihispania.
Asili ya lugha hiyo ni katika nchi ya Uhispania (Ulaya kusini magharibi), lakini kutokana na historia ya ukoloni na ya biashara lugha hiyo imesambaa sana, hasa Amerika ya Kusini na ya Kati.
Lugha iliyozaa Kihispania ni Kilatini cha Waroma wa Kale waliotawala kwa muda mrefu Uhispania. Ndiyo sababu maneno yake yanatokana na Kilatini kwa asilimia 80, lakini pia na Kiarabu kwa asilimia 8.
Kati ya lugha za Kirumi Kihispania ni lugha ya kisasa ambayo ni karibu zaidi na lugha ya kale, isipokuwa Kisardinia na Kiitalia.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.