Chuchunge
From Wikipedia, the free encyclopedia
Chuchunge, chuchungi, vidau, viroho, makule, mikeke au misusa ni samaki wa baharini wa familia Hemiramphidae katika oda Beloniformes ambao taya la chini ni refu zaidi sana kuliko taya la juu (isipokuwa katika spishi za jenasi Chriodorus na Oxyporhamphus).
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Chuchunge | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Chuchunge mabaka-meusi (Hemiramphus far) | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Jenasi 8 na spishi 60, 18 katika Afrika:
| ||||||||||||
Funga
Wanatokea katika maji vuguvugu ya dunia na huogelea karibu na uso wa maji. Huishi baharini hasa lakini spishi kadhaa hukaa katika mito na milango yao. Ingawa sio muhimu sana kwa biashara, samaki hawa wa malisho husaidia uvuvi wa mafundi na masoko ya kienyeji duniani kote. Pia huliwa na samaki wengine mbuai wenye thamani ya biashara, kama vile sulisuli, nguru na papa.