Gedi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Gedi (pia: Gede) ni kijiji cha wakazi 600 kwenye pwani ya Kenya takriban kilomita 16 kusini kwa Malindi. Ni mahali maarufu pa maghofu ya mji wa Waswahili wa Kale ndani ya msitu wa Arabuko-sokole.[1]
Kuna maeneo 116 ya Waswahili yanayonyooka kutoka kusini mwa Somalia mpaka Vumba kuu katika mpaka wa Kenya na Tanzania.[2] kutokana na uvumbuzi wa magofu ya Gedi uliofanywa na wakoloni miaka ya 1920, Gede imejulikana kama mji uliotambulika zaidi na maeneo yake kufanyiwa utafiti zaidi kando na maeneo ya Shanga, Manda, Ungwana, Kilwa na visiwa vya Komoro.