Fransisko Saveri
From Wikipedia, the free encyclopedia
Fransisko Saveri ni jina la kawaida la Francisco de Jasso y Azpilicueta (Javier, Navarra, leo nchini Hispania, 7 Aprili 1506 - kisiwa cha Shangchuan, China, 3 Desemba 1552) alikuwa padri wa Shirika la Yesu, ambalo alichangia kulianzisha pamoja na Ignas wa Loyola.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f9/Conversion_of_Paravas_by_Francis_Xavier_in_1542.jpg/220px-Conversion_of_Paravas_by_Francis_Xavier_in_1542.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/1e/Castillo_javier.jpg/640px-Castillo_javier.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/84/VisionStFrancisBoccacio.jpg/640px-VisionStFrancisBoccacio.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f9/StPierreParis.jpg/640px-StPierreParis.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/ea/Casket_of_Saint_Francis_Xavier.jpg/640px-Casket_of_Saint_Francis_Xavier.jpg)
Baadaye alitangaza Injili katika nchi nyingi za Ulaya, Afrika na Asia hata akawa kati ya wamisionari maarufu zaidi ya historia ya Kanisa.
Alitangazwa na Papa Paulo V kuwa mwenye heri tarehe 25 Oktoba 1619, halafu Papa Gregori XV akamtangaza mtakatifu tarehe 12 Machi 1622.
Anaheshimiwa na Waanglikana na Walutheri pia.