Darubini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Darubini (kutoka Kiajemi: دوربين, dorbin) ni kifaa cha kutazamia vitu ambavyo viko mbali. Kutegemeana na kusudi lake kuna aina mbalimbali:
- Darubini ndogo za mkononi ni vyombo vinavyotumiwa na wapenda mazingira asilia, wawindaji, polisi na jeshi.
- Darubini kubwa hupatikana mara nyingi katika paoneaanga (vituo vya elimuanga); kuna hasa aina mbili:
- darubiniredio hutumiwa pia na wanaastronomia zikikusanya mawimbi ya sumakuumeme zinazofaa kutupa picha za violwa vya mbali sana isizoonekana kwa njia ya nuru ya kawaida. Zinafaa pia kuonyesha tabia za violwa vya angani vya karibu zaidi zisizotambulika kwa njia ya nuru.