![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7b/Saigoncinnamon.jpg/640px-Saigoncinnamon.jpg&w=640&q=50)
Dalasini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Dalasini (kwa Kiingereza cinnamon) ni aina ya kiungo chenye harufu nzuri kilichokaushwa kutoka katika gome la ndani la spishi 6 za miti za jenasi Cinnamomum katika familia Lauraceae inayoitwa mdalasini.[1][2] Gome linaweza kukatwa katika vipande, kuviringishwa katika "vijiti" au kusagwa kuwa ungaunga.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7b/Saigoncinnamon.jpg/640px-Saigoncinnamon.jpg)
Kiungo hiki hutumika katika mapishi ili kuongeza ladha na kuleta harufu nzuri katika chakula. Pia hutumika kutengenezea chai ya dalasini.
Dalasini ni kiambato kikubwa cha michanganyiko mbalimbali ya viungo kama vile aina kadhaa za masala, k.m. masala ya chai na garam masala.