Chawa-mbao
From Wikipedia, the free encyclopedia
Chawa-mbao (kutoka Kiing. woodlouse) ni arithropodi wa nusuoda Oniscidea katika oda Isopoda ya nusufaila Crustacea ambao wana miguu 14. Ingawa watu wengi wanafikiri kwamba chawa-mbao ni wadudu, kwa kweli ni gegereka. Ilhali gegereka wengi sana huishi majini (bahari na maji baridi), chawa-mbao, warukaji-mchanga (oda Amphipoda) na spishi fulani za kaa (oda Decapoda) hupatikana nchini kavu. Spishi za makundi mawili ya kwanza zinapendelea mahali panyevunyevu, mara nyingi karibu na maji. Spishi nyingi za chawa-mbao zinaweza kujiviringa katika umbo la tufe na kwa hivyo huitwa wadudu-donge.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Chawa-mbao | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Chawa-mbao (Ligia oceanica) | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Oda za chini 2, sectio 4:
| ||||||||||||||
Funga