Buzz Aldrin
mwana anga wa Marekani / From Wikipedia, the free encyclopedia
Dr. Edwin Eugene "Buzz" Aldrin, Jr. (*20 Januari 1930) ni rubani na mwanaanga kutoka nchi ya Marekani. Alikuwa mtu wa pili kukanyaga uso wa Mwezi alipofika pamoja na Neil Armstrong kwenye safari ya chombo cha anga cha Apollo 11.
Aldrin na Armstrong walifika mwezini tarehe 20 Julai 1969 wakiwa watu wa kwanza waliomaliza safari hadi gimba la angani tofauti na Dunia yetu.[1]
Aldrin aliwahi kusoma uhandisi mitambo kwenye chuo cha kijeshi cha West Point mnamo 1951. Aliendelea hadi kupokea shahada ya uzamivu ("PhD") katika fani ya usafiri wa angani kwenye Chuo cha Massachusetts Institute of Technology (MIT) mnamo 1963.
Aliteuliwa kwa safari ya kwenda mwezini na kufika pale alipokuwa na umri wa miaka 39.