Bilioni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bilioni (kutoka Kiingereza "billion"[1][2]) ni namba ambayo inamaanisha milioni elfu moja na kuandikwa 1,000,000,000.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/3c/Billion-cubes-new.svg/640px-Billion-cubes-new.svg.png)
Inafuata 999,999,999 na kufuatwa na 1,000,000,001.
Inaweza kuandikwa pia kifupi 1 × 109.
Kiambishi awali giga kinatumika pia kumaanisha mara 1,000,000,000, ingawa katika lugha nyingine nyingi neno linalofanana na "bilioni" linamaanisha milioni milioni (1,000,000,000,000).