Apolo (Biblia)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Apolo (kwa Kigiriki: Ἀπολλώς, Apollos, labda kifupisho cha Apollonius au Apollidorus[1]) alikuwa Mkristo wa karne ya 1 aliyetokea Alexandria[2] katika familia ya walowezi Wayahudi.
Anatajwa mara kadha katika Agano Jipya kama msomi na msemaji fasaha wa lugha ya Kigiriki aliyefanya kazi ya umisionari wakati mmoja na Mtume Paulo huko Efeso na Korintho.
Tangu kale naheshimiwa na Wakristo wa madhehebu mengi kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Februari.