![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/bc/Simone_Martini_048.jpg/640px-Simone_Martini_048.jpg&w=640&q=50)
Antoni wa Padua
From Wikipedia, the free encyclopedia
Antoni wa Padua (kwa jina la kiraia Fernando Martim de Bulhões e Taveira Azevedo; Lisbon, Ureno 15 Agosti 1195 - Padova, Italia 13 Juni 1231) alikuwa padri na mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo, maarufu hasa kwa mahubiri yake yaliyomstahilia heshima ya kutangazwa Mwalimu wa Kanisa.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/bc/Simone_Martini_048.jpg/640px-Simone_Martini_048.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d0/Visione_di_Sant%27Antonio_da_Padova.jpg/320px-Visione_di_Sant%27Antonio_da_Padova.jpg)
Kwa vipawa vyake vya pekee upande wa akili, elimu, busara, kiasi, ari ya kitume na sala hasa, alichangia sana maendeleo ya shirika lake.
Ni mmojawapo kati ya watakatifu wanaoheshimiwa zaidi katika Kanisa Katoliki, pia kwa sababu ya miujiza mingi inayosemekana kupatikana kwa kukimbilia maombezi yake.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Juni[1].
Waamini wengi wanapenda picha zinazomuonyesha akiwa na maua meupe pe, yakimaanisha usafi wa moyo wake, na akimshika mtoto Yesu mikononi, kadiri ya tukio la ajabu lililosimuliwa na vyanzo mbalimbali.