From Wikipedia, the free encyclopedia
Yese au Yishai (kwa Kiebrania: יִשַׁי, Yišay, Yīšáy, maana yake "Mfalme" au "Mungu yupo" au "Zawadi ya Mungu"; kwa Kigiriki: Ἰεσσαί, Iessai; kwa Kilatini: Isai, Jesse) ni mtu anayetajwa na Biblia kama baba wa mfalme Daudi wa Israeli. Huyu pengine anatajwa tu kama "Mwana wa Yese" (Ben Yishai). Hivyo anatajwa pia katika orodha ya vizazi vya Yesu (Math 1:1-17).
Baba yake alikuwa Obedi, mwana wa Boazi na Ruthu. Kama hao wote aliishi Bethlehemu.
Mtu wa kabila la Yuda, alizaa watoto saba wa kiume, Daudi akiwa wa mwisho wao.[1] Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati kinawataja hivi: Eliabu, Abinadabu, Shimea, Nethaneli, Raddai, Ozem na Daudi mbali ya mabinti wawili, Zeruia and Abigaili.[2]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.