Nguva ni wanyama wakubwa wa oda Sirenia wanaoishi baharini. Hata hivyo ni mamalia wanaozaa watoto walio hai na kuwalisha kwa maziwa. Nguva huwa na mikono ya mbele na mkia wenye umbo la pembetatu. Wanaishi kwenye pwani za Bahari ya Hindi, Bahari ya Karibi, Afrika ya Magharibi na mto wa Amazonas. Wanaweza kufikia urefu wa mita 2.5 hadi 4 na uzito wa kg 1,500.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Nguva
Thumb
Nguva wa kawaida
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Nusungeli: Theria
Oda ya juu: Afrotheria
Oda: Sirenia
Illiger, 1811
Ngazi za chini

Familia 2, jenasi 3 na spishi 5:

  • Dugongidae Gray, 1821
    • Dugong Lacépède, 1799
      • D. dugon Müller, 1776
    • Hydrodamalis Retzius, 1794
      • H. gigas (Zimmermann, 1780)
  • Trichechidae Gill, 1872
    • Trichechus Linnaeus, 1758
      • T. inunguis (Natterer, 1883)
      • T. manatus Linnaeus, 1758
      • T. senegalensis Link, 1795
Funga

Wanahatarishwa kutokana na uwindaji hivyo wanalindwa kila nchi.

Jina la Kisayansi Sirenia linatoka na neno la Kigiriki Σειρῆνες Seirēnes. Neno la "nguva" pia ina maana ya mtu mwenye mwili wa mwanamke na mkia wa samaki kama sireni wa mitholojia ya Kigiriki. Hula manyasi ya bahari na mimea ya maji mingine.

Spishi

Picha

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.