Fyekeo[1] (kutoka kitenzi "kufyeka"; kwa Kiingereza scythe) ni zana ya kilimo kwa ajili ya kukata nyasi au nafaka kama ngano. Muundo wake unafanana na mundu lakini kisu na mpini ni mrefu zaidi. Zinamwezesha mtumiaji kukata eneo kubwa kwa urahisi kulinganishwa na matumizi ya mundu au kifyekeo cha kawaida.

Thumb
Fyekeo na mundu.
Thumb
Mchoro ukionyesha mkulima anayetumia fyekeo.

Mtumiaji wake anasimama wakati anakata nyasi. Kisu kinahitaji kunolewa mara kwa mara, hivyo kila mtumiaji hubeba pia jiwe la kunoa.

Fyekeo ilikuwa kifaa kikuu cha kukata nyasi na kuvuna nafaka katika Ulaya, Asia ya Magharibi na Marekani hadi kusambaa kwa mashine zinazotekeleza shughuli hizo. Fyekeo zinatumiwa bado, hasa katika mazingira ambako tabia ya uso wa ardhi hairuhusu matumizi ya mashine.

Katika Afrika matumizi ya fyekeo hayajaenea; inasemekana mara nyingi nyasi za Afrika ni ngumu mno kwa zana hiyo. Hata hivyo kuna majaribio ya kufundisha matumizi yake kwa wakulima wadogo wasio na uwezo wa kugharamia mashine.

Katika Kiswahili neno fyekeo linatumika zaidi kumaanisha "kwanja".

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

Video

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.