From Wikipedia, the free encyclopedia
Poitiers ni mji wa Ufaransa wa Kati kando ya mto Clain wenye wakazi 91 000. Ni mji wa kale unaotembelewa na watalii kwa sababu ya majengo mengi ya kale. Poitiers ndio mji mkuu katika mkoa wa Poitou-Charentes.
Poitiers | |
Mahali pa mji wa Poitiers katika Ufaransa |
|
Majiranukta: 46°34′55″N 0°20′10″E | |
Nchi | Ufaransa |
---|---|
Mkoa | Poitou-Charentes |
Wilaya | Vienne |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 91,395 |
Tovuti: www.mairie-poitiers.fr |
Poitiers ilianzishwa na Wagallia kabla ya uvamizi wa Julius Caesar.
Mmojawapo kati ya watu maarufu wa mji huo ni askofu wake Hilari wa Poitiers, anayeheshimiwa kama mtakatifu, babu wa Kanisa na mwalimu wa Kanisa.
Mwaka 732 mfalme wa Wafranki Karolo Nyundo alishinda jeshi la Waarabu katika mapigano ya Tours na Poitiers na kuzuia uenezi wa dola la Uislamu katika Ulaya ya Magharibi.
Makala hii kuhusu maeneo ya Ufaransa bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Poitiers kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.