From Wikipedia, the free encyclopedia
Osmi (Osmium, kutoka Kigiriki ὀσμή osme, "harufu") ni elementi yenye namba atomia 76. Ni metali ya mpito ngumu na haba sana[1][2]. Alama yake ni Os.
Huwa na utendanaji mdogo na elementi nyingine, hivyo huhesabiwwa kati ya metali adimu.
Inapatikana kwa viwango vidogo katika mbale ya Platini. Osmi ni elementi yenye densiti kubwa katika elementi zote.
Matumizi yake ni hasa katika aloi za platini au iridi kwa vifaa vidogo vinavyohitajika kuwa vigumu na kudumu muda mrefu[3].
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.