From Wikipedia, the free encyclopedia
Mikrobiolojia (kutoka maneno ya Kigirikiμῑκρος, mīkros, "ndogo"; βίος, bios, "uhai"; na λογία, logia, "elimu") ni fani inayochunguza vidubini vyenye seli moja, nyingi au visivyo nayo kabisa.[1] Mikrobiolojia ina matawi yake, yakiwemo virolojia, mukolojia, parasitolojia na bakteriolojia.
Bakteria ziligunduliwa mara ya kwanza na Antonie van Leeuwenhoek mwaka wa 1676, kwa kutumia darubini ya lensi moja ya muundo wake mwenyewe.[2] Aliziita "animalcules" na alichapisha habari za utafiti wake kwenye msururu wa barua kwa Shirika la Muungano wa Mfalme. Jina bacteriam lililetwa miaka mingi baadaye, na Christian Gottfried Ehrenberg katika mwaka wa 1838.[3]
Mwaka 1859 Louis Pasteur alionyesha kuwa mchakato wa kuchachusha unasababishwa na ukuaji wa vijiumbe, na kwamba ukuaji huu si wa kizazi cha kujianzia. (Hamira na kuvu, ambazo kwa kawaida zinahusishwa na uchachushaji, si bakteria, ila ukungu.) Pamoja na mwenzake, Robert Koch, Pasteur alikuwa wa kwanza kuitetea nadharia ya kijidudu ya ugonjwa.[4]
Robert Koch alikuwa mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi wa mikrobiolojia na alishughulikia kipindupindu, kimeta na kifua kikuu. Katika utafiti wake wa kifua kikuu, Koch hatimaye alithibitisha nadharia ya kijidudu, ambayo ilimfanya atunukiwe Tuzo la Nobel mwaka wa 1905.[5] Katika madai yake, Koch aliweka vigezo vya kutathmini kama kiumbe ndicho husababisha ugonjwa, na madai haya yanatumika mpaka leo hii.[6]
Ingawa katika karne ya 19 ilijulikana kwamba bakteria ndizo chanzo cha magonjwa mengi, hakuna matibabu yoyote ya viua-bakteria yaliyopatikana.[7] Katika mwaka wa 1910, Paul Ehrlich alitengeneza kiua vijasumu cha kwanza, kwa kubadilisha rangi ambazo kwa kuchagua zilitia mawaa Treponema pallidum, spirokaeti ambayo husababisha kaswende katika mchanganyiko wa ambao uliua kisababishi magonjwa.[8] Ehrlich alikuwa ametuzwa Tuzo la Nobel mwaka 1908 kwa kazi yake kuhusu elimu ya kingamaradhi, na alianzisha matumizi ya madoa ili kuchunguza na kubaini bakteria, na kazi yake ilijikita kwenye misingi ya doa la Gram na doa la Ziehl-Neelsen.[9]
Mafanikio makubwa katika utafiti wa bakteria yalikuwa kutambuliwa kwa Carl Woese mwaka 1977 kwamba akea zilishuka kutokana na mabadiliko tofauti kutoka yale ya bakteria.[10] Uanishaji huu mpya wa jamii ya filojenetiki ulikitwa kwenye misingi ya kufululizwa kwa ribosomu RNA 16S, na ukagawa prokaryota katika makundi mawili yenye mageuko tofauti, kama mojawapo ya sehemu ya mifumo ya vikoa vitatu.[11]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.