Wilaya ya Kinondoni ni mojawapo ya wilaya 5 za Mkoa wa Dar es Salaam yenye postikodi namba 14000. Kwa lugha nyingine ni manispaa ndani ya jiji la Dar Es Salaam.
Eneo lake ni sehemu za kaskazini za jiji. Kinondoni inaanza upande wa pwani kwenye Selander Bridge juu ya mto Upanga (pia: Msimbazi Creek) na kuendelea kupitia rasi ya Msasani, Kunduchi hadi Mbweni pamoja na hoteli za kitalii zilizopo sehemu hizo.
Barani inaelekea kuvukia barabara ya Morogoro hadi Mbezi na Kibamba. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kipo ndani ya manispaa hii.
Katika sensa ya mwaka 2002, idadi ya wakazi wa Kinondoni ilihesabiwa kuwa 1,775,049 [1]. Baada ya wilaya kumegwa, katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 982,328 [2].
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.