Kipini
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kipini ni kijiji cha wavuvi kwenye pwani ya Kenya katika Kaunti ya Tana River. Iko kilomita 20 kusini mwa Witu kwenye mdomo wa Mto Tana unapoishia katika Bahari Hindi.
Kipini imetambuliwa kuwa mji wa kihistoria ya Waswahili katika Kenya ya leo. [1] Kuna mabaki ya makaburi yaliyojengwa kwa mawe ambayo yanafikiriwa kuwa na asili katika karne ya 11[2].
Katika karne ya 19 Kipini ilitajwa katika mkataba baina ya Ujerumani na Uingereza kama mpaka wa kaskazini wa maeneo ya Sultani wa Zanzibar yaliyotambuliwa nao, mbali na Lamu na miji kadhaa.[3] Hivyo ilikuwa pia kwa muda mpaka wa kaskazini wa koloni la Kenya kwenye pwani[4].
Baadaye wakati wa ukoloni Kipini ilikuwa makao makuu ya wilaya ya Lower Tana.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.