From Wikipedia, the free encyclopedia
Kanga ni ndege wa familia Numididae. Jina hili ni jina la kawaida la ndege hawa, lakini spishi za Afrika ya Mashariki wana majina mengine kama chelele, chepeo, kololo, kororo na kicheleko (tazama orodha ya spishi). Kanga ni wakubwa kuliko kwale na wana rangi nyeusi na madoa meupe. Kichwa chao hakina manyoya lakini spishi tatu zina manyoya juu ya utosi. Kanga mweusi na kanga kidari-cheupe hawajulikani sana, lakini mwenendo wao unasadikiwa kufanana na ule wa spishi nyingine. Hula mbegu, wadudu, makoa na nyungunyungu, na hutaga mayai ardhini. Kanga huwa mwenzi mmoja tu maisha yao yote.
Kanga | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kanga wa kawaida | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Spishi zote zinatokea Afrika. Chepeo hufugwa hususa huko Afrika ya Magharibi na pia katika Ulaya na Marekani.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.