Juliani wa Toledo (Toledo, Hispania, 642 - Toledo, 690) alikuwa mmonaki mwanateolojia aliyehudumia kama askofu mkuu wa Toledo na kuacha kumbukumbu ya umakini katika haki, upendo na juhudi kwa ajili ya wokovu wa watu.

Thumb
Mt. Juliani alivyochorwa.

Aliunganisha Kanisa la rasi ya Iberia na kuendesha sinodi na mitaguso mbalimbali pamoja na kurekebisha liturujia ya Toledo. Pia aliandika sana juu ya mambo mbalimbali akithibitisha imani sahihi.

Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 6 Machi[1].

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Maandishi yake

Viungo vya nje

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.