Bonifas mfiadini
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bonifas (kwa Kilatini Bonifacius, yaani Mtendamema, ambaye aliitwa Wynfrith kabla ya kutajiwa na Papa Gregori II jina hilo jipya; Crediton, Wessex, 673 hivi - Dokkum, 5 Juni 754) alikuwa mmonaki Mbenedikto kutoka Uingereza aliyetumwa kama mmisionari huko Ujerumani (716).




Ili kushinda vipingamizi alikwenda huko Roma akafanywa kwanza askofu (722), baadaye askofu mkuu (732), na baadaye tena balozi wa Papa (738), akijitahidi kuimarisha Kanisa katika dola lote.
Hatimaye akawa mfiadini pamoja na wenzake walau 9 katika Uholanzi wa leo.
Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na wengineo kama mtakatifu, akiitwa pengine "mtume wa Ujerumani"[1].
Sala yake
Mungu wa milele, kimbilio la wanao wote, katika udhaifu wetu ndiwe nguvu yetu, katika giza letu ndiwe mwanga wetu, katika uchungu wetu ndiwe faraja na amani yetu.
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.