Wahadzabe
From Wikipedia, the free encyclopedia
Wahadzabe au Wahadza[1][2] ni kabila la Tanzania linaloishi hasa kandokando ya Ziwa Eyasi kwenye Bonde la Ufa na katika uwanda jirani wa Serengeti.
Leo Wahadza hawafikii 1,000:[3][4] kati yao 300–400 wanaishi bado kwa kuwinda na kuchuma vyakula bila uzalishaji, kama waliofanya mababu wao tangu awali.[5]
Wahadza hawana undugu wa karibu na kabila lingine lolote, na vilevile lugha yao ni ya pekee kabisa.[6][7][8]