![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e4/Marangu19.jpg/640px-Marangu19.jpg&w=640&q=50)
Wachagga
kabila la Kenya na Tanzania / From Wikipedia, the free encyclopedia
Wachagga[1] ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu (lakini pia mchanganyiko wa damu, hasa ya Kikushi) wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e4/Marangu19.jpg/320px-Marangu19.jpg)
Wachagga ni kabila la tatu kwa ukubwa nchini Tanzania.[2] Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi yao ni watu 2,000,000. Hata hivyo kabila hilo ni kama mchanganyiko wa makabila madogomadogo yenye lugha tofauti, jambo la pekee nchini Tanzania.
Shughuli kubwa ya Wachagga ni biashara, kilimo na kazi za ofisini.