Waamoni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Amon (kwa Kiebrania עַמּוֹן ʻAmmôn; kwa Kiarabu a=عمّون|t=ʻAmmūn), ni jina la kabila la zamani lililotawala upande wa mashariki wa mto Yordani, leo nchini Yordani.[1][2][3]
Mji muhimu zaidi wa Waamoni ulikuwa Rabbah au Rabbath Ammon, mahali pa Amman ya leo, makao makuu ya Jordan.
Waliabudu hasa Milkom na Molekh (pengine ni majina mawili ya mungu yuleyule).
Kwa mara ya mwisho uwepo wao unatajwa katika kitabu cha karne ya 2.