Viti maalum vya wanawake
From Wikipedia, the free encyclopedia
Viti maalum vya wanawake ni nafasi bungeni zinazotolewa kwa utaratibu unaopatikana katika nchi mbalimbali na unaolenga kuongeza idadi ya wanawake na athira yao katika bunge na mabaraza na kwa njia hiyo katika siasa ya nchi hizo kwa jumla.
Kuna nchi nyingi za dunia zilizochukua hatua za kuongeza nafasi za wanawake serikalini kulingana na mkataba kuhusu ufutaji wa ubaguzi wote wa wanawake (Convention on the Elimination of All Forms of Discrimination Against Women) uliosainiwa na mataifa 189 tangu kuanzishwa mwaka 1981 na kuimarishwa na azimio la Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2011. [1].