Upanga Magharibi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Upanga Magharibi ni kata ya Wilaya ya Ilala katika Mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania, yenye postikodi namba 11103.
Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 11,845 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2002, kata ya Upanga Magharibi ilikuwa na wakazi wapatao 9,259 waishio humo [2].
Kata ya Upanga magharibi, kiutawala, ina mitaa mitatu:
- Mtaa wa Charambe ambao ndipo ilipo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
- Mtaa wa Mfaume ambao ndipo ilipo ofisi ya makao makuu ya SIDO Tanzania
- Mtaa wa Fire ambao ndipo kituo kikubwa cha Idara ya Zimamoto.