From Wikipedia, the free encyclopedia
Tukani (kwa Kilatini na Kiingereza Tucana) [1] ni jina la kundinyota kwenye nusutufe ya kusini ya dunia yetu.
Tukani iko karibu na ncha ya anga ya kusini. Inapakana na makundinyota Nyoka Maji (Hydrus), Zoraki (Phoenix), Kuruki (Grus), Mhindi (Indus) na Thumni (Octans).
Tukani inapatikana kati ya makundinyota yaliyobuniwa tangu mabaharia Wazungu walipozunguka Dunia yote katika karne ya 16 na kuona mara ya kwanza nyota za kusini. Hazikujutajwa katika vitabu vya Wagiriki wa Kale au vya Waarabu. Kundinyota hili lilielezwa mara ya kwanza na mabaharia Waholanzi Pieter Dirkszoon Keyser na Frederick de Houtman katika safari yao ya kuelekea Indonesia zikaonyeshwa mara ya kwanza mwaka 1598 katika atlasi ya nyota ya Petrus Plancius.
Keyser alitumia jina la Kiholanzi "Den Indiaenschen Exster" alipotumia neno la kwake nyumbani kwa kutaja Hondohondo aliyoona katika nchi za Bahari ya Hindi. Ndege hii haikujulikana bado katika Ulaya lakini alifanana na Tukani ya Amerika ya Kusini na hivyo Petrus Plancius alitumia jina hili katika globu yake ya nyota aliyotengeneza baada ya kupokea taarifa ya Keyser na Houtman; jina hili lilisambazwa zaidi na Johannes Bayer katika atlasi ya nyota “Uranometria” likawa jina la kimataifa.
Leo iko pia katika orodha ya makundinyota 88 ya Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [2]. Kifupi chake rasmi kufuatana na Ukia ni 'Tuc'.[3]
Nyota angavu zaidi ni α Alfa Tucanae yenye mwangaza unaoonekana wa mag 2.86 ikiwa umbali wa Dunia wa miaka nuru 199[4]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.