![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/9d/Flag_of_TANU.svg/langsw-640px-Flag_of_TANU.svg.png&w=640&q=50)
Tanganyika African National Union
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tanganyika African National Union (TANU) kilikuwa chama kilichotawala Tanganyika na Tanzania hadi muungano wa chama hiki na Chama cha Afro-Shirazi cha Zanzibar ulipounda Chama cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/9d/Flag_of_TANU.svg/320px-Flag_of_TANU.svg.png)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/sw/thumb/9/9f/Takadir_-_Nyerere.jpg/320px-Takadir_-_Nyerere.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/sw/thumb/8/8f/WAZEE_WA_TANU.jpg/640px-WAZEE_WA_TANU.jpg)
Ukweli wa haraka Uendo, Ukoloni ...
Funga
TANU ilianzishwa 7 Julai 1954 kutokana na Tanganyika African Association (TAA). TAA ilikuwa na mwelekeo wa kitamaduni zaidi ya siasa. Mwenyekiti wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Kambarage Nyerere.
TANU ilishinda kila uchaguzi chini ya utawala wa kikoloni ikawa chama cha kuongoza Tanganyika hadi ilipopata uhuru wake mwaka 1961. Katiba ya Taifa ya mwaka 1962 ilifanya TANU kuwa chama cha pekee nchini ikifuata mfano wa nchi za kijamaa zenye muundo wa siasa ya chama kimoja.