![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/bc/African_Blue_Flycatcher_-_Kibale_-_Uganda_06_4453_%252819438571632%2529.jpg/640px-African_Blue_Flycatcher_-_Kibale_-_Uganda_06_4453_%252819438571632%2529.jpg&w=640&q=50)
Chechele (Stenostiridae)
Ndege wadogo wa familia Stenostiridae / From Wikipedia, the free encyclopedia
Chechele ni ndege wa familia Monarchidae na Stenostiridae. Zamani wale wa Stenostiridae waliainishwa katika familia Muscicapidae (Culicicapa), Monarchidae (Elminia), Sylviidae (Stenostira) na Rhipiduridae (Chelidorhynx), lakini uchunguzi wa ADN umeonyesha kwamba wana mnasaba na kwa hivyo wamepewa familia yao.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Chechele | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Chechele buluu | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 4, spishi 9:
| ||||||||||||||
Funga
Wana rangi ya buluu (Elminia), ya kijivu (Stenostira) au ya manjano (Chelidorhynx na Culicicapa). Wanatokea misituni au porini kwa vichaka katika Afrika na Asia. Hula wadudu. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika panda ya matawi. Jike huyataga mayai 2.