![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f6/Osaka07_D9A_W4-100_VC.jpg/640px-Osaka07_D9A_W4-100_VC.jpg&w=640&q=50)
Sherone Simpson
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sherone Simpson (alizaliwa 12 Agosti 1984) ni mwanariadha wa nchi ya Jamaika ambaye huiwakilisha nchi yake katika mashindano ya kimataifa. Alishinda medali ya dhahabu katika mbio ya 4 x 100m katika mashindano ya Olimpiki ya 2004 na medali ya fedha katika Mashindano ya Mabingwa wa Dunia ya 2005.Alishinda medali ya fedha katika mbio ya 100m katika Olimpiki ya 2008 baada ya kukimbia kwa muda mmoja na mwenzake wa Jamaika ,Kerron Stewart. Muda wake wa kibinafsi wa 10.82 s katika mbio ya 100m,Simpson ndiye mwanariadha mwanamke wa nne bora nchini Jamaika.Mbele yake ni Merlene Ottey,Shelly-Ann Fraser na Kerron Stewart. Muda wake bora wa 22.00 s katika mbio ya 200m ndio muda wa nne bora katika orodha ya Jamaika akiwa nyuma ya Merlene Ottey,Grace Jacson,Juliet Cuthbert,Veronica Campbell-Brown na Kerron Stewart. Amekimbia mbio ya 200m na muda huu mara mbili. Kocha wa Simpson ni Stephen Francis mjini Kingston.Jamaika, anaposoma katika Chuo Kikuu cha Teknolojia. Yeye ,pia, alisoma katika shule ya Manchester High.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/f6/Osaka07_D9A_W4-100_VC.jpg/640px-Osaka07_D9A_W4-100_VC.jpg)
Rekodi za medali | ||
---|---|---|
Riadha ya Wanawake | ||
Anawakilisha nchi :Jamaika | ||
Michezo ya Olimpiki | ||
Dhahabu | 2004 Athens | 4 x 100 |
Fedha | 2008 Beijing | 100m |
Mashindano ya Mabingwa wa Dunia ya IAAF katika Riadha | ||
Fedha | 2005 Helsinki | 4x100 m |
Michezo ya Jumuia ya Madola | ||
Dhahabu | 2006 Melbourne | 200 m |
Dhahabu | 2006 Melbourne | 4 x 100 m |