Samarkand
From Wikipedia, the free encyclopedia
Samarkand (kwa Kiuzbeki na Kirusi: Самарқанд; kwa Kiajemi: سمرقند) ni mji maarufu wa kihistoria katika Asia ya Kati. Ni mji wa pili kwa ukubwa katika Uzbekistan na mji mkuu wa Mkoa wa Samarkand.
Samarkand ilikuwa mapema mji muhimu ikiwa kituo kwenye barabara ya hariri (Silk Road) iliyounganisha China na nchi za Asia ya Magharibi na Ulaya.
Baada ya uenezi wa Uislamu ilikuwa kitovu cha Kiislamu kilichovuta wataalamu wengi.
Katika karne ya 14, ilikuwa mji mkuu wa milki ya Timur (Tamerlane) na ndiyo mahali pa kaburi lake linalojulikana kama "Gur-e Amir". Msikiti wa Bibi-Khanum bado ni mojawapo ya majengo maarufu zaidi ya mji.
Mwaka 2001, UNESCO iliingiza Samarkand katika orodha yake ya Urithi wa Dunia kama "Samarkand - Njiapanda ya Tamaduni".