Ratili
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kwa sarafu ya Uingereza, angalia makala ya Pauni (sarafu)
Ratili (kutoka Kiarabu رطل ratl; pia: pauni kutoka Kiingereza pound) ni jina la kizio cha uzito wa takriban nusu kilogramu.[1] Wakati wa ukoloni chini ya mfumo wa vipimo rasmi vya Uingereza wakati ule pound ilikuwa kipimo rasmi kilicholingana na gramu 454. Kifupi chake kilikuwa £ au lb kutoka Kilatini libra.
Tangu kuenea kwa vipimo vya SI ratili imetazamiwa kama jina la takriban gramu 454.