![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b6/Yucatan_peninsula_250m.jpg/640px-Yucatan_peninsula_250m.jpg&w=640&q=50)
Rasi ya Yucatan
From Wikipedia, the free encyclopedia
Yucatan (tamka yu-ka-tan) ni rasi kubwa huko Amerika Kaskazini (au Amerika ya Kati, inategemea kama unaiona pekee na kaskazini). Rasi hii inatenganisha Bahari ya Karibi na Ghuba ya Mexico.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b6/Yucatan_peninsula_250m.jpg/640px-Yucatan_peninsula_250m.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/bb/Maya_Languages.png/320px-Maya_Languages.png)
Sehemu ya kaskazini ya rasi hiyo iko ndani ya Meksiko, ikigawiwa katika majimbo yake ya Yucatan, Campeche na Quintana Roo. Kusini ya rasi iko katika Guatemala na Belize. Upande wa mashariki kipo kisiwa kikubwa zaidi cha Meksiko ambacho ni Cozumel.
Kasoko ya Chicxulub iko kwenye pwani ya kaskazini. Ilisabishwa na pigo la asteroidi miaka milioni 65 iliyopita iliyoleta maafa makubwa duniani pamoja na kuangamizwa kwa dinosauri.