Kisiwa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kisiwa ni eneo la nchi kavu kati ya bahari, ziwa au mto linalozungukwa na maji wakati wote. Ukubwa wake hautoshi kukifanya kiitwe "bara".
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d2/Ball%27s_Pyramid2.jpg/250px-Ball%27s_Pyramid2.jpg)
Visiwa vilivyo karibu kama kundi mara nyingi huitwa "funguvisiwa".
Tofauti kati ya kisiwa kikubwa na bara dogo limeamuliwa kati ya
- Greenland inayoitwa kisiwa kikubwa duniani chenye eneo la kilomita za mraba milioni 2.1 na
- Australia inayotazamwa kuwa bara dogo duniani lenye eneo la kilomita za mraba milioni 7.7.