![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/7b/Marbled_lungfish_1.jpg/640px-Marbled_lungfish_1.jpg&w=640&q=50)
Kambaremamba
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kambaremamba ni samaki wa maji matamu walio na mapafu na kwa hivyo wanaweza kupumua hewa. Pia wana mapezi yenye nyama na mifupa iliyokuzwa vizuri. Hutokea katika mito, maziwa, vinamasi na mabwawa. Mara nyingi wanaishi katika mashimo ndani ya sakafu. Wanaweza kuendelea kuishi katika mashimo hayo hata ikiwa maji yakikauka, isipokuwa kambaremamba wa Australia.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kambaremamba | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Kambaremamba wa Afrika (Protopterus aethiopicus) | ||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
| ||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||
Familia 2, jenasi 3, spishi 6:
| ||||||||||||
Funga