Wagadugu
mji mkuu wa Burkina faso / From Wikipedia, the free encyclopedia
Wagadugu (kwa Kifaransa huandikwa Ouagadougou) ni mji mkuu wa Burkina Faso, na pia mji mkubwa kabisa wa nchi hiyo na wa mkoa wa Centre.
Ukweli wa haraka Nchi, - Wakazi kwa ujumla ...
Jiji la Wagadugu | |
Nchi | Burkina Faso |
---|---|
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 2,453,496 |
Funga
Mwaka 2019 idadi ya wakazi ilikuwa milioni 2,453,496, lakini mji unakua haraka.
Wagadugu iko katika jimbo la Kadiogo. Kuna ofisi za serikali na viwanda kadhaa vya nguo na vyakula.
Mji ni pia kitovu cha usafiri na mawasiliano. Kuna kiwanja cha kimataifa cha ndege na njia ya reli kwenda Abidjan (Côte d'Ivoire), halafu barabara za kwenda Lome (Togo), Bamako (Mali), Niamey (Niger), Accra (Ghana).
Wagadugu ina chuo kikuu kilichokuwa chuo cha mwanahistoria maarufu Joseph Ki-Zerbo.
Tamasha la kimataifa la filamu za Afrika (FESPACO) hufanyiwa Wagadugu.