From Wikipedia, the free encyclopedia
Omar Brown (alizaliwa 21 Juni 1982 katika mji wa Trelawny) ni mwanariadha wa nchi ya Jamaika ambaye ni mtaalam katika mbio ya 200m.
Yeye alikuwa na mafanikio mengi akiwa mwanariadha kijana huku akishinda medali ya fedha na shaba katika mbio za 200m na 100m katika Mashindano ya Mabingwa vijana wa Dunia katika mwaka wa 1999. Mwaka uliofuata alichukua nafasi ya nne katika Mashindano ya Mabingwa Vijana wa Dunia. Aliwakilisha Chuo Kikuu cha Arkansas katika mashindano kati ya vyuo vikuu.
ALishinda mbio ya mita 200 katika Michezo ya Jumuia ya Madola ya 2006, akaorodheshwa kama nambari tisa duniani katika mbio ya mita 200 katika mwaka huo na gazeti la Track and Field News.
Katika mwaka wa 2007, yeye alimwoa mwanariadha wa Olimpiki wa Jamaika, Veronica Campbell. Yeye alipata jeraha mwaka huo kwenye kifudio. Alirudi kushiriki katika mbio za majaribio za Jamaika za 2008 lakini akapata jeraha jingine mguuni kutokana na kukimbia katika mtindo tofauti.Alikimbia kwa njia tofauti kwa kuwa alikuwa na maumivu kwenye kifudio. Alifanyiwa upasuaji mnamo Septemba 2008 kurekebisha shida fulani lakini kovu tishu iliyobaki ilimzuia kurudi kushiriki katika mbio. Hakurudi hadi mwisho wa msimu wa 2009 alipochukua nafasi ya nne katika mbio ya mita 200 katika Shindano la Shanghai Golden Grand Prix.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.