From Wikipedia, the free encyclopedia
Nape Moses Nnauye ni mwanasiasa Mtanzania na mwanachama wa chama cha kisiasa cha CCM. Alihudumia kama katibu wa itikadi wa CCM. Amechaguliwa kuwa mbunge wa Mtama kwa miaka 2015 hadi sasa. [1]
Aliteuliwa na rais Magufuli kuwa waziri wa habari, utamaduni na michezo. Mwaka 2017 aliondolewa uwaziri baada ya kuagiza uchunguzi wa tendo la Paul Makonda, mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam aliyewahi kuvamia ofisi za kituo cha habari cha binafsi cha Clouds[2][3]. Alipojaribu kujieleza mbele ya wanahabari alizuiwa na maafisa wa usalama waliotoa bastola na kumwamuru asiseme kitu.[4][5]
Baada ya kutokea kwa taarifa kuwa alishiriki katika majidiliano ya kumkosoa rais, kwenye mwaka 2019 alikutana na rais Magufuli akaomba kusamehewa akapata kibali cha rais[6].
Katika uchaguzi wa mwaka 2020 alirudi bungeni. Kwenye Januari 2022 ameteuliwa na rais mpya Samia Suluhu Hassan kuwa waziri wa Wizara ya Habari na Teknolojia ya Habari.[7]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.