Nabii Obadia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nabii Obadia (jina la Kiebrania lenye maana ya "Mtumishi wa YHWH) alikuwa nabii wa Israeli ya Kale baada ya Yerusalemu kutekwa na kuteketezwa na Wababuloni (586 KK hivi).
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/80/Abdias.jpg/320px-Abdias.jpg)
Alitoa utabiri wa mistari 21 tu dhidi ya Edomu ambayo inaunda kitabu cha nne kati ya 12 vya Manabii Wadogo.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 19 Novemba[1][2].