From Wikipedia, the free encyclopedia
Mzee ni mtu aliyeishi miaka mingi baada ya kuzaliwa.
Katika jamii za Kiafrika, sawa na jamii nyingi duniani, neno "mzee" linatumiwa pia kama cheo cha heshima kwa kumtaja mtu mwenye mamlaka fulani.
Hapo kuna hoja ya kuwa mtu aliyeendelea katika umri anawazidi vijana kwa hekima na maarifa pia, kwa hiyo anafaa kutawala au kufanya maazimio au angalau kutoa ushauri.
Kimapokeo tamaduni nyingi duniani zinajua heshima ya mzee. Hapo kiongozi anateuliwa kati ya wazee.
Halmashauri ya wazee ni bodi ya kufanya maazimio muhimu. Mkutano wa wazee ni mahali pa kuchukua rufaa, kwa hiyo ina kazi inayolingana na mahakama kuu katika jamii zenye taasisi hizo.
Wazee ni watu wanaotunza mila na desturi pamoja na kumbukumbu ya historia na wanapaswa kusikilizwa kwa heshima.[1]
Katika jamii zilizopangwa kwa rika (vikundi kulingana na umri), kama Wamasai au Wazulu, rika la wazee linapaswa kusikilizwa katika maazimio yanayohusu jamii yote.
Wakati umri unazidi na wazee wanakuwa dhaifu ugumu unaanza kuendelea na cheo cha heshima. Hata hivyo wote wanapaswa kuonyesha heshima kwao hata kama hali halisi hawatajali tena ushauri wao.
Tatizo hilo ni tofauti kati ya tamaduni za kimila ambako watu dhaifu hawaishi muda mrefu sana kutokana na uhaba wa nafasi za tiba upande mmoja na tamaduni zilizoendelea ambako nafasi za tiba zinawezesha watu wengi kufikia umri mkubwa ambako asilimia inaanza kupoteza akili au uwezo wote wa kutembea kwa miaka mfululizo.[2] Kama idadi ya wazee dhaifu mno inazidi ni vigumu kuendelea na hoja ya heshima kwa wazee.
Matumizi ya kulingana ya maneno yenye maana ya "mzee" yanapatikana kwa lugha mbalimbali:
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.