![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/76/Lava_Lake_Nyiragongo_2.jpg/640px-Lava_Lake_Nyiragongo_2.jpg&w=640&q=50)
Mlima Nyiragongo
Volcano ya Kongo / From Wikipedia, the free encyclopedia
Mlima Nyiragongo ni volkeno yenye mwinuko wa mita 3,470 juu ya UB [1] iliyopo kwenye Milima ya Virunga iliyopo mpakani mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda. Mlima Nyiragongo ni sehemu ya Hifadhi ya Virunga ukiwa kilomita 12 upande wa kaskazini mwa miji ya Goma (Kongo) na Gisenyi (Rwanda).
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/76/Lava_Lake_Nyiragongo_2.jpg/640px-Lava_Lake_Nyiragongo_2.jpg)
Kwenye kilele cha mlima kuna kasoko yenye upana wa kilomita 2 iliyojaa ziwa la lava (zaha), yaani miamba ya moto yaliyo katika hali ya kiowevu.
Ziwa hilo la lava la Nyiragongo wakati mwingine limekuwa ziwa la lava kubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni. Kabla ya mlipuko wa mwaka 1977 lilikadiriwa na kina cha mita 600 kilichoshuka na kupanda tena.[2] [3] Mlima Nyiragongo na mlima jirani wa Nyamuragira ilikuwa chanzo cha karibu nusu ya milipuko yote ya volkeno katika historia inayojulikana barani Afrika. [4]